Sehemu Ya 1
Mtunzi..... MoonBoy
Simu No. +255714419487 WhatsApp
www.facebook.com/Chombezo-Media-571095712946246/
Ilipoishia Jana
THE MEAT OF MY MOTHER
Inapoanzia Rasmi ni hapa sehemu ya kwanza
____________________________________
Simulizi yetu inaanzia msituni ikiwa ni mida ya jioni, yapata kama saa 12.30 hivi za jioni, alionekana dada mmoja wa makamo akiwa anahema sana huku akikimbia, nikisema msitu namaanisha msitu kwelikweli,.. Dada huyo alikuwa akikimbia mithili ya mtu anaetaka kuepusha maisha yake, kana kwamba kuna mtu au kitu kilichokuwa kikimkimbiza katika msitu huo,....
"uuuuuu nakufa jamaniiii"
Ni sauti ya dada huyo mwenye umri mkubwa tu, akiwa kama anaomba msaada katikati ya miti, majani, migomba, miba, na vingine vingi vipatikanavyo msituni,.. Lakini Kiukweli hakukua na mtu wala kitu kilichokuwa kikimkimbiza,... Alisimama mahali na kujifanya kama kajificha katika migomba iliostawi mpaka kuweka kiza kinene katika msitu huo, haijulikani alikuwa akikimbizwa na nini,...
Lakini ghafla anaanza tena kukimbia kana kwamba kamuona adui wake aliokuwa akimkimbiza katika msitu huo,
Mdada huyo hakufika mbali alinyongwa na kamba za miguu na kudondoka chini, sasa akawa hawezi hata kuamka hivyo akawa anapiga tu kelele kana kwamba mtu anaemfukuza yupo jirani yake, ila kwa jinsi tunavyo ona hakukuwa na mtu.. Lakini ghafla akiwa katika hali ya kujinasua,.... Alifika huyo aliekuwa akimkimbiza,......
"uuuuuuuuuuuuuwiiiiiii"
Alipiga kelele kubwa kuashiria hatari ya kudhuriwa na kitu fulani kisicho julikana.....
Lakini kumbe haikuwa live bali ni mama mmoja aliokuwa akiwaza katika kichwa chake, na haikuwa ndoto na wala hakuwa kalala, bali ni fikra zake ndizo zilizomfanya kufikiri kitu kama hicho.. Mama huyo alikurupuka hapo kitandani na kukimbilia sebuleni,... Ila kwa wakati huo hapo nyumbani palikuwa ni mapema sana yapata kama saa saba za mchana, lakini katika fikra zake za msituni ilikuwa ni saa 11.30 jioni,.. Mama huyo alitoka nje na kuangaza huku na kule kama kuna kitu atakiona,... Lakini ghafla kamuona mschana mmoja hivi anamfahamu vizuri tu,
"amizati mwanangu hujambo"
Aliongea mama huyo kana kwamba ni salamu kwa mschana huyo
"sijambo mama shikamoo"
"marahaba mwanangu.. Karibu ndani"
Mama huyo alimkaribisha amizati (ami) ndani, na amizati kazoea sana katika nyumba hio ila sio kwao sasa hatujui hapo ni kwa akina nani...
"mama? suhaibu kaenda wapi"
Aliuliza ami huku aking'ata vidole vyake bila kusahau uzuri aliokuwa nao,.. Ni mtoto wa Kiislamu na mwenye maadili mazuri ya kuitwa mke
"huyu mtoto hata sijui kaenda wapi, mana leo ni Jumamosi"
"au atakuwa kaenda kwa mwalimu wake"
"angeniambia, mana kila anapokwenda lazima aniage"
"basi atarudi mama"
"ni sawa"
"mama huna kazi hapa nikusaidie"
Aliongea ami, ila kwa Muonekano tu ami ni mpenzi wa kijana wa huyu mama, sasa kijana mwenyewe wala bado hatujamwona wala kumtambua....
"ahsante sana mwanangu, Kiukweli sina, kazi zote nimesha zimaliza"
"sawa mama ila kama ipo nipe tu nifanye"
"usijali mwanangu ami..... Ila ami, kuna kitu nataka kukuuliza kuhusu mahusiano yenu"
Ami alishtuka sana kuskia mama huyo akitaamka maneno hayo...
"uliza tu mama"
"hivi, ulisha wahi kukutana na suhi"
Aliuliza mama, kitu ambacho amizati alikishangaa sana..
"una maana gani mama"
"sina maana mbaya ami,.. Nataka kujua tu"
"nd, nd, nd, ndio mama"
Amizati alikubali kuwa alishakutana na suhi kimapenzi,.... SUHI ni kifupi cha SUHAIBU ambaye ni mtoto wa kiume wa huyu mama,
"hivi mnatumiaga zana"
"ndio mama, na hua anasisitizia sana swala hilo, kitu ambacho mimi sipendi mama"
Mama suhi alikasirika kidogo kwa maneno ya amizati,..
"kwanini hupendi mtumie kinga"
"mama, najua suhaibu bado ni mwanafunzi, lakini mimi sio mwanafunzi... Natamani sana nilee mtoto wake"
"amizati utanichefua sasa... Kwanini unataka kuniharibia mtoto wangu"
"mama, sina maana hio... Suhi ni mume wangu mtarajiwa"
"hivi hujui kuwa ukizaa kabla ya kuoana huyo mtoto atakuwa haram,.. Kwanini unashindwa kufikiria.."
"basi Nisamehe mama,.. Mimi nilifikiri Unapenda ujukuu"
"hata mimi sihitaji kwa sasa mpaka mwanangu amalize shule"
Aliongea mama huyo tena kwa jazba la hali ya juu sana,..
"basi mama Nisamehe sana, sikujua ila tunatumia sana kinga"
"ndio nataka iwe hivyo"
Mama hataki mtoto wake awe na mtoto kwa wakati huo, mana bado anasoma, tena ni mwanafunzi mwenye akili nyingi kuliko wote Tanzania nzima, yaani nzima kabisaaa...
Tukija huku alipo suhaibu,.. Kweli ni mtoto mwenye akili, tena ni hensamu kupitiliza, yaani kama ni wale wauza sura, basi suhaibu ni mmoja wao, tena namba moja... Wakati kule nyumbani wanawaza suhi kaelekea wapi, kumbe alikwenda tuisheni kujikumbushia, mana leo ni siku ya Jumamosi... Akiwa ndani ya gari la head mistress (mkuu wa shule wa kike) suhi alikuwa akiendesha gari hio wakati wa kitoka tuisheni yaani huyu mama anatoa masomo ya ziada kwa wanafunzi wake, tofauti na masomo ya wiki nzima... Na hua sio bure inatoka pesa kubwa ndipo mtoto wako akubaliwe kusoma masomo ya ziada kwa siku ya Jumamosi,...
Mwalimu huyo alikuwa siti ya kushoto mana suhi yeye ndio dereva, lakini mwalimu alikuwa akimwangalia sana kijana huyo, tena mbaya zaidi alikuwa kama anamtamani kimapenzi mana suhaibu kajaaliwa sura na bodi zuri la kimapenzi...
Wakati huo suhi yupo bize na usukani wa gari,... Walifika katika nyumba moja nzuri sana
"piiiii piiiii"
Suhaibu alipiga honi ili geti lifunguliwe, na kweli haikupita hata dakika mbili geti likafunguliwa,..
Walipofika ndani sahi alishuka na kutoa mkoba wa mwalimu na kumpa mfanyakazi wa ndani, yaani house girl ili aingie nao ndani,
"ticha?.. Naomba nikuage"
Aliongea Suhaibu huku akiinamisha sura yake chini, na wakati huo kavua miwani ya giza na kofia iliounganika na sweta, yaani alivaa sweta lenye kofia kwa juu (plover)....
"unakwenda wapi sasa saa nane yoye hii"
Aliongea mwalimu huyo huku akimtaka Suhaibu aingie ndani,..
"ingia ndani upate hata kinywaji"
Suhaibu akaona sio vizuri kweli kuingia kwa mwalimu wake na kutoka bure,.. Suhi aliingia na kukaa katika sofa,.. Head mistress ni mwanamke mtu mzima, au tuseme jimama la nguvu, yaani katika mijimama basi head mistress ni bonge la jimama yan,... Sihi alikaa lakini ana aibu sana.... Kiujumla ni mtoto aliotulia na asiependa makuu katika maisha ya sasa...
"nikupatie kinywaji gani"
Mwalimu alimuuliza mwanafunzi wake,
"mmhh chochote tu mwalimu"
Aliongea suhi huku mwalimu akifungua friji ili amchagulie suhi kinywaji kizuri zaidi,... Lakini sasa friji likiwa wazi, suhi alitoa macho makali sana kana kwamba kuna kitu kaona kwenye friji hilo, wakati mwalimu anachagua kinywaji suhi kaamka kitofauti kabisa na kuelekea kwenye friji hio,.. Suhaibu ni mtoto mwenye aibu sana lakini friji ilipofunguliwa tu aibu yote ilimtoka,... Sasa udenda unamtoka kwa kitendo cha friji kuwa wazi
GHARAMA YANGU NI SHARE 200 TU,
ZITAKAPOFIKA TU, NAENDELEZA...
www.facebook.com/Chombezo-Media-571095712946246/
STORI ZANGU ZOTE HIZI HAPA....
(1).KIJAKAZI WA KIUME
(2).MLINZI WA GETI
(3).DEREVA TOYO
(4).MTOTO WA HAYATI
(5).ONE DAY YES
(6).SECONDARY SCHOOL
(7).FUNDI CHEREHANI
(8).MWIGIZAJI BALAYA
(9).THE DOM
(10).THE ISLAMIC WIFE
(11).MKE JEURI
(12).YOUNG PASTOR
(13).MUUZA CHIPSI
(14).WAPANGAJI WENZANGU
(15).NYAMA YA MAMA
KUZISOMA ZOTE, BONYEZA HAPA
www.facebook.com/Chombezo-Media-571095712946246/
AU.... NICHEKI KUPITIA NAMBA +255714419487 WhatsApp
Utazipata Zote Mpaka Mwisho Kwa Simu No: +255714419487 WhatsApp, Au, Like Page Yetu Ya Facebook Kwa Kubonyeza Hapa Chini ili Usipitwe
www.facebook.com/Chombezo-Media-571095712946246/
tAfBoy {.Tanzania's Frugal Boy..}
